Web - Amazon

We provide Linux to the World


We support WINRAR [What is this] - [Download .exe file(s) for Windows]

CLASSICISTRANIERI HOME PAGE - YOUTUBE CHANNEL
SITEMAP
Audiobooks by Valerio Di Stefano: Single Download - Complete Download [TAR] [WIM] [ZIP] [RAR] - Alphabetical Download  [TAR] [WIM] [ZIP] [RAR] - Download Instructions

Make a donation: IBAN: IT36M0708677020000000008016 - BIC/SWIFT:  ICRAITRRU60 - VALERIO DI STEFANO or
Privacy Policy Cookie Policy Terms and Conditions
Kenya - Wikipedia

Kenya

From Wikipedia

Jamhuri ya Kenya
Bendera la Kenya Coat of Arms of Kenya
Bendera Nembo
Hadabu ya Taifa: Harambee
(Kiswahili:
Kiingereza, pull together
Location of Kenya
Lugha za Taifa Kiingereza
na Kiswahili
Mji Mkuu Nairobi
Rais Mwai Kibaki
Eneo
 - Jumla
 - 2.3% Maji
Kadiriwa 46 duni
582,650 km²
Acha
Umma
 - Kadiriwa ( 37 duni )
 - Jumla (32,021,856 )
 - Umma kugawa na Eneo 53.4
Kadiriwa 37 duni
4,561,599
4,298,269
38/km² ([[Orotha ya nchi kulingana na chumo cha umma kugawa na eneo|142 duni])
GDP (PPP)
 - Jumla
 - kwa kipimo cha umma
81 kadir
33,028 (151)
917 (151)
Uhuru
 - Kadirifu
 - Barabara
Kutoka Uingereza)
  Disemba 12
  1963
Fedha Shilingi ya Kenya_KES
Saa za Eneo UTC +3
Wimbo wa Taifa Ee Mungu Nguvu Yetu
Intaneti TLD .ke
Codi ya simu 254

Jamhuri ya Kenya, ama Kenya ni nchi katika Afrika ya Mashariki. Imepakana na Ethiopia upande wa kaskazini, Somalia upande wa kaskazini-mashariki, Tanzania upande wa kusini, Uganda upande wa magharibi, na Sudani upande wa kaskazini-magharibi, na upande kusini-mashariki ni Bahari Hindi.

Kenya ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na Umoja wa Afrika.

Contents

[edit] Jiografia

Kenya iko kusini na kaskazini ya Ikweta. Eneo lake limepasuliwa na Bonde la Ufa. Sehemu ya juu ndiyo mlima wa Mlima Kenya (5199 m), sehemu ya chini ni ufukoni wa Bahari Hindi.

Mito mikubwa: Tana, Athi na Kerio.

Miji mikubwa: (idadi za 2005): Nairobi 2.750.561, Mombasa 799.727, Nakuru 259.934, Eldoret 218.472, na Kisumu 216.479.

Eneo la Kenya ni 582,650 km². Nyanda za Juu za Kenya ni mojawapo za eneo zinazojulikana kuwa na ukulima mwenye mavuno zaidi Afrika.

Hali ya hewa ni ya kupoa kwenye Nyanda za Juu, ya joto pwani na katika nyanda za chini.

Kenya ina maeneo makubwa mazuri ambayo hayajaendelea
Kenya ina maeneo makubwa mazuri ambayo hayajaendelea
Times Tower, Makao makuu ya Watoza ushuru wa  Kenya, Ambayo iko Nairobi, Kenya.
Times Tower, Makao makuu ya Watoza ushuru wa Kenya, Ambayo iko Nairobi, Kenya.

[edit] Historia

Tako la Kifungu: Historia ya Kenya

Visukuku viligunduliwa Afrika ya Mashariki miaka ya karne hii, imesekana miaka milioni 20 iliyo ya kale Kijibinaadam katembea eneo hii. Hivi Karibuni ziwa la Turkana limeonyesha kwamba Visukuku za Kijibinaadam kama Homo habilis na Homo erectus viliishi eneo ya Kenya kutoka mika milioni 2.6 iliyopita.

Historia ya Ukoloni wa Kenya, ni kutoka kipindi cha wabeberu wa Kijerumani kuthibitisha kutawala eneo la Sultani wa Zanzibari na mali yake yote ya pwani mwaka wa 1885, baadaye kampuni ya kibeberu ya Waingereza ya Afrika Mashariki ikafuata Wajerumani mwaka 1888. Ubishano wa mabeberu ukatokea na Ujerumani kamwachia Uingereza pwani yote na mali, mwaka wa 1890. Hii ilifuatiwa na ujenzi wa reli ya Kenya-Uganda kupitia bara. Reli hii, ilipingwa kwa vita vikali na kabila la Wanandi, wakiongozwa na Orkoiyot Koitalel arap Samoei kwa miaka kumi, karne ya 1895 hadi 1905. Lakini Waingereza waliendelea kujenga reli na kupenya bara. Imeaminika ya kwamba Wanandi ndiyo Wafrika wa kwanza kupinga ujenzi wa reli.

Miaka ya mbele karne 1900, milima ya kati nchini Kenya ilikuwa na masetla wakulima Waingereza na Wazungu wengi wakulima ambao walitajirika kwa kupanda kahawa. Lakini mwaka wa 1930s wastani wa masetla 30,000 waliishi eneo hilo na kupewa nguvu ya kisiasa kwa sababu ya nguvu zao za kiuchumi. Eneo hiyo tayari ilikuwa nyumbani mwao Wagiǐkǔyǔ ambao walikuwa kadri ya milioni moja. Kwa sheria za Kizungu kabila lenyewe halikuwa na hati za kumiliki ardhi, hivyo wazungu kwa ulinzi wakibinafsi wakawafinyilia kwa kuwakataza wenyeji kupanda kahawa, na pia kutoza ushuru wa nyumba na ambao hawakuwa na mashamba wakawa wakiwafanyia Wazungu kazi ili kupata makao. Wengi wa Wagikuyu walihamia mjini ili kupata makao ama kazi.

Kutoka oktoba 1952 mbaka Disemba 1959, Kenya ilikuwa kwa HALI YA HATARI kwa sababu ya mapambano ya kudai ardhi yao yaliyoongozwa na Mau Mau kupinga utawala wa Waingereza. Gavana wa Waingereza, aliitisha jeshi kutoka Uingereza na jeshi ya Kiafrika ya "Bunduki za Mfalme". Januari 1953, Meja Jenerali Hinde alipishwa kama rubani wa kuzuia jamaa za wakereketwa. Lakini hali ya hatari ilibaki moto moto kwa ukosefu wa udadisi kwa hivyo Jenerali Sir George Erskine akawekwa kama Kamanda Mkuu (Amri)wa jeshi yote ya ukoloni Mai 1953, kwa usaidizi na kuungwa mkono na Winston Churchill. Kwa kumshika Warǔhiǔ Itote (General China) 15 Januari 1954, alihojiwa kinyenya na hivyo basi Amri ya Mau Mau kueleweka. Operesheni Anvil ilifunguliwa tarehe 24 April 1954 baada ya wiki kadhaa kupangwa na Jeshi na uwamuzi wa baraza ya Vita. oparesheni iliweka Nairobi kwa mazingiwa ya Jeshi, na watu kuangaliwa na watetezi wa Mau Mau kuwekwa kizuizuni. Mai 1953 pia askari Gadi Wanyumbani aliweza kutambuliwa kama afisa wa serikali. Afisa wa Gadi wa Nyumbani alikuwa mtiifu kwa Waingereza na kwa hivyo alitumiwa kama jama ya kupinga Mau Mau kuliko Jeshi ya Waingereza ama Waafrika wa Bunduki za Mfalme. Mwisho wa HAlI YA HATARI Gadi wa Nyumbani alikuwa ameuwa karibu 4,686 Mau Mau, asilimia 42% kwa jumla ya wakereketwa. Kushikwa kwa Dedan Kimathi tarehe 21 Oktoba 1956 huko Nyeri ilileta Mau Mau kushidwa na kupoa na kuwacha umakuruhi wakijeshi.

Kura ya kwanza ya Wafrika kwa Bunge ya wakoloni kama baraza la wanasheria ilitokea mwaka mnamo 1957. Hata kama Waingereza walitaka kuwaachia Wafrica Kadirifu nguvu za kisiasa, ilikuwa ni chama (Kenya Afrika National Union) KANU -Wafrika Wakenya wa Umoja Wataifa Jomo Kenyatta, Aliunda serikali kabla ya Kenya kupata Uhuru 12th December 1963. Mwaka mmoja baadaye, Kenyatta akawa Rais wa kwanza Kenya. Kenyatta Kufariki mwaka 1978, Daniel arap Moi akawa Rais, nakushinda kura kwa democracia mwaka 1992 mpaka 1997, tena kura ya pili mpaka 2002, Moi alifikakiwango na sheria ya Katiba kuendelea Urais na Kustaafu Kabarak , na Mwai Kǐbakǐ, kupata kura na muungano wa Upinzani "National Rainbow Coalition" - NARC, na kuchaguliwa Rais. Upiga Kura Uliamliwa na Wananchi na Wangalizi waulimwengu kuwa kura za Uhuru na Amani ambao ni maendeleo ya demokrasia Kenya.

[edit] Siasa

Tako la kifungu: Siasa za Kenya

Sanamu ya Jomo Kenyatta mbele ya Mahakama Kuu ya sheria
Sanamu ya Jomo Kenyatta mbele ya Mahakama Kuu ya sheria

Kenya ni Jamhuri; na Rais wa Kenya ni Kiongozi wa Serikali napiya Kiongozi wa Bunge. Kenya ikonabaraza la taifa la wenyekiti ama Wanabunge 210 ambao wachaguliwa kwa kura kwa kipindi cha miaka mitano kuakilisha makao au divisheni yao. Na piya kuna Wenyekiti 12 ambao wamechaguliwa bila kura na vyama za wanabunge kulingana naukubaliano wa Vyama. Rais yuamchagua Makamu wa Rais na Mawaziri kutoka wenyekiti waliochaguliwa kwa baraza ya Taifa (Bunge). Mwanasheria Mkuu na Msema wa Bunge hao siyo maafisa Wabunge wao ni Afisa wa serikali. Sheria inaongozwa na Mahakama Kuu ya kenya ambayo chifu ni Hakimu Mkuu akiongoza Mahakimu wa Mahakama Kuu ya Kenya napiya Majaji wa Mahakama ya Rufaa. Hakimu wote wameteuliwa na Rais.

Kenya ni Nch ya Vyama vya sisa kadir kutoka mwaka 1991 ambapo katiba ilitekelezwa, na wanasiasa kupindukapinduka kwa Vyama ilikupata muungano wakudhamiri kisiasa. Disemba mwaka 2002, Kenya ilifanya kura fumbuzi na zakimadaraka za Kidemokrasia na kumchagua Mwai Kǐbakǐ kama Rais na Chama- muungano wa taifa demokrasia ama NAK. NAK na Chama- wazingatifu demokrasia (Kenya) LDP waliunda Muungano wa chama NARC ambayo inatawala sasa Kenya. muungano huo ulileta wanasiasa wenye hekima zaidi kama (Msomi). Kilemi Mwiria, aliyepata usomi wake wa digirii kuu kwa Chuo Kikuu cha Stanford. alikuwa piya Karani Generali wa Ushirika wa Walimu wa Chuo Kikuu (UASU).

Kenya hasa iko kwa njia ya kutoa katiba ya kutoka siku za ukoloni na kuandika Katiba mpya. katiba iliopo kutoka siku za ukoloni ilirekebishwa mara kadhaa na kumpa Rais nguvu nyingi za kisiasa hata kumkinga Rais kuhukumiwa na sheria ambayo ilileta ufisadi kwa kila idara. Utekelezaji wa Katiba bado unabishano kwa Muungano wa Kisisa ambao unatawala Nchi. Siasa za kulia- Nak wanataka Rais mwenye Mamlaka ya Bunge na Serikali lakini Siasa za Kushoto LDP -- wakiongozwa na Raila Odinga -- waitaka Bunge ikiongozwa na Waziri Mkuu. Julai 2005 serikali kaamua kutekeleza Katiba iliyopishwa na Jumuiya ya Katiba huko Bomas na kutangaza Kura ya maoni kwa katiba, Novemba 21 2005. Ambapo ilikataliwa na wachanguzi. Wachaguzi ilikuwa warushe kura kuiunga mkono Katiba hiyo ama Kuikataa.

[edit] Muundo wa Serikali

Ramani ya mikoa ya Kenya
Ramani ya mikoa ya Kenya

Nchi ya Kenya imegawiwa katika mikoa minane kila mmoja ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa ambaye amepewa mamlaka na Rais. Mkoa mwenyewe nao umegawiwa katika Wilaya zinazogawiwa kwa Tarafa. Nazo tarafa zimegawiwa kwa mitaa na kugawiwa zaidi kwa vijiji. Eneo ya Nairobi ni maalum ni Mkoa mwenye wilaya moja tu. Serikali yasimamia mikoa na wilaya zote.

  1. Bonde la Ufa
  2. Mashariki
  3. Kaskazini-Mashariki
  4. Magharibi
  5. Nyanza
  6. Kati
  7. Pwani
  8. Nairobi*

[edit] Uchumi

Tako la Kifungu: Uchumi wa Kenya

Nguvu ya Uchumi wa Kenya unapatikana kwa Utalii na Ukulima. Uchumi umeanza kuonyesha ukuzi baada ya vilio. Watu wengi wabisha kuwa Uchumi ulikuzwa kwa uvivu kwasababu ya ufukara wa usimamizi na ukosefu usawa wa ugeuzi wa uchumi; Wengine wakasema nikwasababu ya bei ya vifaa kuanguka na kushidwa kupenya soko za kuuza za Dunia ya magharibi.

Mwaka wa 1993, Serikali ya Kenya iliweka kipindi cha uchumi Kukarimisha Uchumi na Ugeuzi unahusu kutoa: vyeti vya kununua ng'ambo,Kuelekeza bei, na Kuelekeza biashara za Fedha. Hii yote ilifanyika na igemeo la Banki Kuu ya Dunia, (IMF) Ikopeshi Mataifa Fedha, na wakopeshi wengine. Ugeuzi huo ulileta maendeleo ya uchumi ukuzi uvivu miaka ya 1990s. Mambo mengine ya Serikali kuwacha kuendesha na kuelekeza bei na Fedha za kigeni. Mktasari wa Serikali ni kwamba Ugeuzi wa Uchumi ni wamaana kwa sababu kutogeuza vile kulile Ufisadi (Ukora) wa kuuza dhahabu na almasi ng'ambo Ambapo Serikali ya Kenya Ilipoteza Milioni 600 za Dolla za Marekani. Hii ilileta Shilingi dhaifu na Uchumi Mvivu na maendeleo pungufu.

Kenya GDP ilikuzwa asilimia 5% mwaka 1995 na asilimia 4% mwaka wa 1996.


 
Mikoa ya Kenya
Bendera ya Kenya
Bonde la Ufa | Kaskazini-Mashariki | Kati | Magharibi | Mashariki | Nairobi | Nyanza | Pwani|


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia
Our "Network":

Project Gutenberg
https://gutenberg.classicistranieri.com

Encyclopaedia Britannica 1911
https://encyclopaediabritannica.classicistranieri.com

Librivox Audiobooks
https://librivox.classicistranieri.com

Linux Distributions
https://old.classicistranieri.com

Magnatune (MP3 Music)
https://magnatune.classicistranieri.com

Static Wikipedia (June 2008)
https://wikipedia.classicistranieri.com

Static Wikipedia (March 2008)
https://wikipedia2007.classicistranieri.com/mar2008/

Static Wikipedia (2007)
https://wikipedia2007.classicistranieri.com

Static Wikipedia (2006)
https://wikipedia2006.classicistranieri.com

Liber Liber
https://liberliber.classicistranieri.com

ZIM Files for Kiwix
https://zim.classicistranieri.com


Other Websites:

Bach - Goldberg Variations
https://www.goldbergvariations.org

Lazarillo de Tormes
https://www.lazarillodetormes.org

Madame Bovary
https://www.madamebovary.org

Il Fu Mattia Pascal
https://www.mattiapascal.it

The Voice in the Desert
https://www.thevoiceinthedesert.org

Confessione d'un amore fascista
https://www.amorefascista.it

Malinverno
https://www.malinverno.org

Debito formativo
https://www.debitoformativo.it

Adina Spire
https://www.adinaspire.com