Afrika Kusini
From Wikipedia
|
|||||
Wito la taifa: /Xam: !ke e: ǀxarra ǁke (English: "Unity In Diversity" or literally, "Diverse People Unite") |
|||||
Wimbo wa taifa: National anthem of South Africa | |||||
Mji mkuu | Cape Town (Bunge) Pretoria (Serikali) Bloemfontein (Mahakama Kuu) |
||||
Mji mkubwa nchini | Johannesburg | ||||
Lugha rasmi | Kiafrikaans, Kiingereza, Kizulu, Kixhosa, Kiswati, Kindebele, Kisotho cha kusini, Kisotho cha Kaskazini, Kitsonga, Kitswana, Kivenda | ||||
Serikali
Rais
|
Jamhuri Thabo Mbeki |
||||
Uhuru Maungano ya Afrika Kusini |
31 Mei 1910 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
1,221,037 km² (ya 25) kidogo sana |
||||
Idadi ya watu - Julai 2005 kadirio - 2001 sensa - Msongamano wa watu |
47,432,000 [1] (ya 26) 44,819,278 39/km² (ya 136) |
||||
Fedha | Rand (ZAR ) |
||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC+2) not observed (UTC+2) |
||||
Intaneti TLD | .za | ||||
Kodi ya simu | +27 |
||||
1.) angalia: Makadirio ya idadi ya watu ni pamoja na vifo kutokana na UKIMWI. |
Afrika Kusini ni nchi kubwa ya Afrika ya Kusini yenye wakazi takriban milioni 45. Imepakana na Namibia, Botswana, Zimbabwe, Msumbiji na Uswazi.
Mji mkubwa ni Johannesburg. Wajibu wa mji mkuu yamegawiwa kwa mji mitatu: Cape Town ni makao ya Bunge, Pretoria ni makao ya Serikali na Bloemfontein ni makao ya Mahakama Kuu.
Nchi ina majina rasmi 11 kutokana na lugha rasmi 11. Ndizo Kiafrikaans, Kiingereza, Kizulu, Kixhosa, Kiswati, Kindebele, Kisotho cha kusini, Kisotho cha Kaskazini, Kitsonga, Kitswana, Kivenda.
Kati ya watu mashuhuri sana wa Afrika Kusini ni Nelson Mandela aliyekuwa rais kati ya 1994 hadi 1999. Wengine ni Christian Barnaard (daktari wa kwanza duniani aliyetumia moyo wa mtu kwa mtu mwingine) na Shaka Zulu aliyekuwa kiongozi wa kijeshi kabla ya ukoloni.
[edit] Uchumi
Kiuchumi Afrika Kusini ni nchi yenye pande mbili kabisa. Sehemu ya uchumi ina hali ya kimaendeleo kabisa ikiwa viwanda na huduma za Afrika Kusini zinalingana na hali ya juu kabisa duniani na hali ya maisha ya wananchi waliomo katika sekta hii inalingana na nchi kama Australia au Ulaya ya magharibi. Kwa upande mwingine hali ya maisha ya sehemu kubwa ya wananchi ni umaskini kama katika sehemu nyingine za Afrika au Uhindi wa mashambani. Lakini kwa ujumla hali ya maisha iko juu kuliko nchi nyingi za Afrika.
Sekta muhimu za uchumi ni migodi ya kuchimba dhahabu au almasi, viwanda na huduma kama benki au bima.
[edit] Jeshi
Jeshi la Afrika Kusini ina silaha za kisasa kushinda nchi zote za majirani. Uchumi unawezesha nchi ya kutumia kiasi kikubwa kwa ajili ya jeshi kuliko nchi zote za Afrika kusini ya Sahara.
Afrika Kusini iliwahi kuwa na silaha za kinyuklia lakini ilizibomoa baada ya mwaka 1993.
[edit] Viungo vya nje
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia |