Winston Churchill
From Wikipedia
Winston Leonard Spencer Churchill (30 Novemba, 1874 – 24 Januari, 1965) alikuwa mwanasiasa, mwanajeshi na mwandishi kutoka nchi ya Uingereza. Mara mbili alikuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, miaka ya 1940-45, na 1951-55. Mwaka wa 1953 alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fasihi.