Réunion
From Wikipedia
Région Réunion | |
---|---|
Image:Blason ile reunion 1925.jpg | |
Jina la Kifaransa | Région Réunion |
Jina la kawaida | Reunion |
Mji Mkuu | Saint-Denis |
Eneo | 2,512 km² |
Mkuu wa Mkoa | Paul Vergès (PCR) (tangu 1998) |
Idadi ya wakazi | 706,300 |
Sensa ya mwaka | 1999 |
Wakazi kwa km² | 309 |
Wilaya (arrondissements) | 4 |
Ramani Reunion na Ufaransa bara |
Réunion (Kifaransa: La Réunion) ni kisiwa cha Kiafrika na mkoa wa ng'ambo wa Ufaransa (Kifaransa: département d'outre-mer, au DOM) katika Bahari Hindi upande wa mashariki wa Madagaska. Kisheria hali yake ni sawa na mikoa mingine ya Ufaransa hivyo ni pia sehemu ya Umoja wa Ulaya.
Contents |
[edit] Eneo lake
Reunion iko 800 km upande wa mashariki wa Madagaska. Pamoja na visiwa vya Mauritius na Rodrigues ni sehemu ya visiwa vya Maskareni. Kisiwa kina eneo la 2.512 km² kikiwa na upenyo wa 50 hadi 70 km. Milima mikubwa ni ya kivolkeno. Upande wa mashariki wa kisiwa ndipo mlima wa "Piton de la Fournaise" mwenye 2611 m uliolipuka zaidi ya mara 100 tangu kumbukumbu ya kimaandishi ilianzishwa mwaka 1640. Mlipuko wa mwisho hadi leo ilikuwa tar. 4.10.2005. Mlima wa "Piton des Neiges" ndio mkubwa kisiwani ikiwa na 3070 m juu ya UB.
[edit] Hali ya hewa
Hali ya hewa ni ya joto mwaka wote. Majira ya mvua ndiyo kati ya Disemba hadi Machi.
[edit] Historia na Utawala
Taarifa za kwanza za kimaandishi hudokeza ya kwamba kisiwa ilikuwa bila wakazi. Waarabu waliita "dina margabin" yaani kisiwa cha magharibi. Mbaharia Mreno Diego Dias alifika tar. 9.02.1513 ambayo ni sikukuu ya Mt. Apolonia katika desturi ya kikatoliki na kukiita kisiwa kwa jina la mtakatifu huyu "Santa Apolonia" jinsi inavyoonekana katika ramani za kwanza. Baadaye Wareno walitumia jina la nahodha maarufu Pedro de Mascarenhas na kujumlisha visiwa vya Reunion, Mauritius na Rodrigues kwa jina la visiwa vya Makareni. Visiwa hivi vilikuwa na umuhimu fulani kama vituo vya kupumzika katika safari kati ya Ulaya na Bara Hindi mabaharia wakitafuta maji ya kunywa, nafasi ya kutengeneza jahazi zao na kuongeza chakula. Lakini hapakuwa na makao ya kudumu kisiwani.
[edit] Utawala wa Kifaransa
Mwaka 1640 Wafaransa walivamia kisiwa na kukitangaza kuwa mali ya Ufaransa. Walikiita "Île Bourbon" kutokana na jina la familia ya wafalme wa Ufaransa. Mwaka 1665 walowezi wa kwanza Wafaransa walianza kujenga nyumba zao. Ufalme ulipoondelwa wakati wa mapinduzi ya Ufaransa kisiwa kimepewa jina jipya la Reunion tar. 17.03.1793. Wakati wa Vita za Napoleoni ndio Waingereza waliovamia kisiwa mwaka 1810 lakini kukirudisha kwa Wafaransa baada ya vita 1815.
[edit] Uchumi wa mashamba na watumwa
Walowezi wazungu walianzisha mashamba kwa ajili ya mahitaji ya jahazi zilizopita. Kuanzia mwaka 1718 mazao ya biashara yalilimwa , kwanza kahawa baadaye pia vanilla na hasa sukari. Kwa kusidi hiyo watumwa walipelekwa Reunion kutoka Afrika bara, Bara Hindi na Madagaska. Mwaka 1768 kisiwa kilikuwa na 26,284 wakazi huru hasa Wafaransa na watumwa 45,000. Ufaransa ulitia sahihi maazimio ya Mkutano wa Vienna 1815 pamoja na kumaliza biashara ya watumwa lakini biashara hii iliendela kwa siri na kupanuka hasa wafungwa kutoka Afrika. Idadi ya watumwa iliendela kuongezeka hadi kuondolewa hali ya utumwa tar. 20.12.1848. Baada ya mwisho wa utumwa walowezi walitafuta wafanyakazi huko Bara Hindi wakachukua wafanyakazi Wahindi wasiofika kama watu huru kwa miaka na haki kidogo. Baadaye hata wafanyakazi Wachina walichukuliwa.
[edit] Mkoa wa Ufaransa
Mwaka 1946 Reunion ilipewa cheo cha Mkoa wa Ufaransa, tangu 1997 imekuwa sehemu ya Umoja wa Ulaya. Mkoa wa Reunion ina wilaya (Kifaransa: arrondissements) nne.
[edit] Wakazi
Wakazi wanaonyesha historia hii katika mchanganyiko wao wa aina za watu na tamaduni kutoka pande mbalimbali wa dunia. Sehemu kubwa ya wakazi ni watoto wa watumwa au wafanyakazi wasio huru wa zamani wakinonyesha tabia za Wahindi, Waafrika na Wachina. Takriban robo ya wakazi ni wa asili ya Ulaya. Vikundi hivi havikai mbali kuna mchanganyiko wa kila aina. Wakazi wengi hufuata Ukristo wa kikatoliki, wengine Uislamu na Uhindu. Kuna pia Waprotestanti.
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad |Cote d'Ivoire | Djibouti | Eritrea | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesoto | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Uhabeshi | Uswazi | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya kiafrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Ufaransa: Mayotte · Réunion | Hispania: Visiwa vya Kanari · Ceuta · Melilla | Ureno: Visiwa vya Madeira | Uingereza: · Kisiwa cha St. Helena · Kisiwa cha Diego Garcia |