Rosa Parks
From Wikipedia
Rosa Parks (Februari 4, 1913 – Oktoba 24, 2005) anakumbukwa kwa uamuzi wake wa kukataa kumpisha kiti Mmarekani mweupe kama sheria ilivyosema wakati huo. Uamuzi wake huo hapo mwaka 1955 ulipelekea mzozo uliosababisha Mgomo wa Mabasi wa Montgomery na kuchangia katika Vuguvugu la Haki za Kiraia Marekani. Baada ya kitendo chake cha kukataa kumpa mtu mweupe kiti ndani ya basi na Mgomo wa Montgomery uliodumu kwa mwaka, Mahakama ya Marekani ilitamka kuwa sheria za ubaguzi ndani ya mabasi huko Alabama na Montgomery zilikiuka katiba.