Alcuin Mtakatifu
From Wikipedia
Alkuin (mnamo 732 – 19 Mei, 804) alikuwa mtaalamu mkuu wakati wa enzi ya Karoli Mkuu. Alizaliwa karibu na mji wa York kule Uingereza ambapo alikuwa mwalimu mkuu wa shule ya Kanisa Kuu kwa miaka mingi. Mwaka wa 781 alisafiri Italia na kumkuta mfalme Karoli aliyemwalika kuwa mwalimu katika kitala chake kule mji wa Aachen. Huko Alkuin alianzisha chuo kilichohudhuriwa hata na Karoli Mkuu mwenyewe na familia yake. Kupitia chuo hicho elimu iliboreshwa na shule nyingi zilianzishwa katika ufalme mzima. Mwaka wa 796 Alkuin alitoka Aachen kwenda mji wa Tours ambapo alikuwa mkuu wa watawa mpaka kifo chake.