Niamey
From Wikipedia
Niamey ni mji mkuu wa Niger. Iko mwambaoni wa mto Niger. Ikiwa na wakazi 674,950 (sensa ya 2002) Niamey ni mji mkubwa wa Niger na kitovu cha kiutawala, kiuchumi na kiutamaduni.
Kilimo katika mazingira yya mji kina karanga kama mazao ya sokoni; kuna viwanda vya matofali, saruji na nguo.
Niamey ilikuwa kijiji kikaanza kukua tangu Ufaransa ulijenga hapa kituo cha kijeshi tangu miaka ya 1890 BK. Mwaka 1926 ikawa mji mkuu wa koloni ya Niger. Mwaka 1930 ilikuwa na wakazi 3,000, wakati wa uhuru mwaka 1960 na wakazi 30,000 na mnamo 1980 na wakazi 250,000.