Tiba
From Wikipedia
Tiba (au: Uganga) ni elimu kuhusu magonjwa ya watu mwilini na rohoni, jinsi ya kuzuia magonjwa na kuhusu njia ya kurudisha uzima. Elimu hii inafuata mbinu za kisayansi tofauti na uganga wa kienyeji au wa kimila.
Watu wanaoshughulika magonjwa wa watu huitwa tabibu au waganga. Mara nyingi watu huwaita "daktari" lakini neno hili lamaanisha zaidi cheo cha kufaulu chuo kikuu kwenye ngazi ya juu; mara nyingi waganga husoma hadi cheo cha daktari ya tiba.
Watu wanaofanya kazi pamoja na tabibu ni muuguzi (nesi) na wasaidizi wengine.
Tiba imeendelea kiasi cha kuwa na masomo yake madogo yanayoangalia hasa magonjwa ya sehemu fulani ya mwili tu. Kila somo ndogo lina wataalamu wake kwa mfano tiba ya moyo, ya ngozi, ya viungo vya ndani, ya upasuaji, ya wagonjwa wa watoto na kadhalika.
Makala hiyo kuhusu "Tiba" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Tiba kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |
Categories: Tiba | Mbegu